Wednesday, 12 March 2014

Hizi picha zilizonaswa na satelite ya China zikionyesha mabaki kama ya ndege baharini. Fuatilia hapa na vitendo.

Serikali ya China imechapisha picha zilizonaswa na mtambo wake wa satelite zikionyesha mabaki ya kitu kipana kikielea katika bahari ya Kusini mwa China. Picha hizo zilipigwa siku ya Jumapili, saa ishirini na nne baada ya ndege ya abiria ya Malaysia kutoweka ikiwa na abiria 239, lakini haijabainika kama vifaa hivyo ni vya ndege hiyo.