Thursday, 27 August 2015

Bibi aeleza jinsi mjukuu wake alivyotafunwa na ngono kinyume na maumbile

Ulishawahi kufikiria ni kwa kiasi gani ufanyaji wa mapenzi kinyume na maumbile unaweza kumwathiri mtoto wa kike? Ni kitendo kinachoweza kusababisha kifo kwa mlengwa.

Ni mama wa makamo aliyekutwa akimsimulia mwenzie kile kilichomkuta mjukuu wake aliyekuwa akifanya mapenzi kinyume na maumbile na mume wake kwa muda mrefu.

Mama huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa mjukuu wake huyo alikuwa na mazoea ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile na mume wake.

Alianza kufanya tendo hilo tangu muda mrefu kiasi kwamba tabia hiyo ilijenga mazoea na kuwa mchezo ambao hakuweza kuuacha.

Ilifikia kipindi yeye na mume wake waepuka kupata ujauzito wakihofia kupata shida wakati wa kujifungua.

 Kwa mujibu wa mama wa mjukuu huyo, wakati wa uhai wake, mjukuu huyo alishatoa mimba karibia sita akishirikiana na mume wake.

Siku za mwizi ni harobaini, kwenye chezacheza yao ujauzito ukapatikana. Bila shaka mchakato wa kuichoropoa ulishindikana na kuamua kuiacha.

Wakati wa kujifungua ulipofika, mjukuu huyo alishikwa na uchungu na kupelekwa hospitali tayali kwa kujifungua.

Inasemwa kwamba wakati wa kujifungua, njia sahihi ambayo mtoto alitakiwa apitie ikagoma kufunguka. Cha ajabu njia ya haja kubwa ndio iliyokuwa inafunguka.

Baada ya kufahamu nini kinaendelea madaktari waliokuwa wanamhudumia mjukuu walishauli kuwa anatakiwa afanyiwe upasuaji kwa kuwa mjukuu huyo hawezi kujifungua kwa njia ya kawaida.

Ndugu wa mjukuu walijulishwa na kukubaliana na ufanywaji wa upasuaji ili kuokoa maisha ya mtoto wao. 

Baada ya upasuaji, mjukuu alirudi nyumbani na mtoto wake huku akiwa na kibarua cha kuuguza kidonda cha upasuaji.

Baada ya siku kadhaa baadae, mjukuu alianza kuharisha mfululizo chanzo kikiwa ni njia yake ya haja kubwa kulegea kutokana na ufanyaji wa mapenzi kinyume na maumbile.

Siku kadhaa baadae mjukuu alizidiwa na homa na kufariki dunia na kuacha mtoto wa miezi kadhaa.