Saturday, 22 August 2015

Mabloga acheni kuchapisha picha za utupu mtandaoni

Ilidhaniwa kuwa ukuaji wa teknolojia ungeweza kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta ya habari lakini badala yake teknologia hii inageuzwa kuwa chanzo cha kuichafua sekta ya habari kwa baadhi ya watu kuchapisha na kusambaza picha na video za ngongo kwenye mitandao ya kijamii kwa kutumia blog.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la mabloga wanaojihusisha na uchapishaji wa picha na video za ngono suala ambalo linadhalilisha tasnia ya habari.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii haswa Facebook kumekuwa kimbilio la mabloga wengi wanaochapisha picha na video za ngono katika blog zao na kuzituma mtandao.

Watu hawa wachache wanaotumia blog zao kuchapisha picha zisizo na maadili kwa jamii wanapelekea mabloga wengine wasafi kudharauliwa huku wakijumuishwa kwenye kundi la wale wavunjifu wa maadili.

Kwa nini tuendeshwe na teknolojia badala ya sisi tuiendeshe teknolojia ili tujitengenezea misingi mizuri ya maendeleo.

blog ni chombo kizuri ambacho kikitumika vizuri kinaweza kuleta faida kadha wa kadha kwa mtumiaji. Inaweza kuwa kama sehemu mojawapo ya kujiiingizia kipato, pia ni sehemu nzuri ya kufanyia mazoezi ya uandishi haswa kwa wale wanaopenda kufanya uandishi.

Sasa kwa nini kijana ufungue blog na kuanza kuchapisha picha na video za ngono? Unajichelewesha, kuna mengi unayoweza kuyafanya kutumia blog yako na kufikia mafanikio.

Acha kupoteza muda kwa kuchapisha picha chafu mtandaoni, igeuze blog yako kuwa chombo cha ukombozi.



Image result for blogger image