Saturday, 12 April 2014

Mugabe aitukana Nigeria.

Balozi wa Zimbabwe nchini Nigeria ameitwa akajieleze kwa sababu ya matamshi ya Rais Robert Mugabe kuhusu rushwa.

Mwezi uliopita Rais Mugabe alilalamika kuwa Wazimbabwe wanaanza kuwa kama Wanigeria wakitaka jambo lifanyike inabidi watie mkono mfukoni.

Wizara ya mashauri ya nchi za nje ya Nigeria imemwambia balozi wa Zimbabwe, Stanley Kunjeku, kwamba hawajafurahishwa na jambo hilo la kuwatusi.