Wanasayansi wa Uchina wamefaulu katika tiba yao mpya ya majaribio ya kutibu upofu.
Walitumia nguruwe katika majaribio hayo ya tiba ya kuondoa upofu, ambapo walitumia konea kutoka kwa wanyama hao.
Sasa wamesema wana imani kwamba hilo litafaa sana kutokana na uhaba wa konea za binadamu.
Inakisiwa kuwa Wachina wapatao 5 milioni wanakabiliwa na matatizo ya konea, sehemu ya mbele ya jichoiliyo ngumu na inayowezesha miali ya mwanga kupenya.
Lakini ni konea 5,000 pekee ambazo hupatikana kila mwaka.
Matatizo ya konea husababisha watu wengi kuwa kipofu.Njia hiyo mpya ya kutibu upofu imeanza kutumiwa baada ya kuidhinishwa na serikali mwaka jana.Konea kutoka kwa nguruwe hutibiwana kutolewa bakteria na virusi, pamoja na kutolewa DNA ya nguruwe, kabla ya kupandikizwa katika jicho la mwanadamu.
Wakosoaji wa mpango huo wanasema Uchina inaenda kwa kasisana, bila kuangazia madhara ya mpango huo kwa kipindi kirefu.